Banza Stone mwana wa Masanja achonga na Mafia Kisiwani na kudai kuwa yupo fiti na atarudi hivyo mashabiki wake wasichoke kumsubiri. Haya ni maswali mafupi aliyohojiwa na Mafiakisiwani.
Mafiakisiwani: Banza mashabiki wako wanakuuliza upo wapi na unafanya nini?
Banza: Nipo ila kuna mambo fulani yalikuwa yananiweka vibaya ila siku si nyingi nitaweza kusikika tena na mashabiki wangu.
Mafiakisiwani: Vipi madai ya kuwa unaumwa na uzushi wa kifo?
Banza: Kwakweli ndio maana naitwa Makaveli kwakuwa kila siku nazushiwa kifo lakini kama unavyoniona,mimi ni mzima wa afya njema.
Mafiakisiwani: Banza unasumbuliwa na nini hasa kwasababu tunaona tu kwenye vyombo mbalimbali vya habari kuwa unaumwa,nini hasa kinachokusumbua?
Banza: Nasumbuliwa na kichwa pamoja na malaria na si kinginecho.
Ma: Je mashabiki wako wategemee nini kutoka kwako?
Banza: Wategemee kitu special,nitatoa wimbo maalumu kwa wale wote wanaonisema vibaya.
Mafiakisiwani: Asante Banza
Tuesday, August 4, 2009
Nipo fiti…Banza Stone!
Posted by Mafia Kisiwani at 12:40 PM
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment