Tuesday, May 26, 2009

TANZANIA,TANZANIA,OH TANZANIA!!


Naomba nikuulize swali; Kwenye muziki unapenda zaidi ujumbe uliomo au midundo kwa maana ya beats? Kwako wewe muziki ni nini? Usiharakishe kunijibu. Fikiri kwanza.

Wakati unafikiri ngoja nikupe jibu langu.Mara nyingi huwa napenda wimbo wenye ujumbe. Midundo ikiwa imetulia huwa nazama pia.Ndio maana nampenda sana Oliver Mutukudzi(mwanamuziki kutoka Zimbabwe) wakati mara nyingi sielewi anachokiongelea mpaka pale ninapopewa tafsiri. Napenda jinsi anavyocharaza gitaa lake na kutawala jukwaa. Napenda muziki kwa sababu naamini muziki ni universal language(lugha ya dunia).

Miongoni mwa nyimbo ambazo nimezisikia hivi karibuni na kupenda ujumbe na midundo ni kutoka kwa mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania anayekwenda kwa jina Roma(pichani). Jina la wimbo wake ni Tanzania. Msikilize Roma kwa kubonyeza player hapo chini kisha uniambie kama ujumbe uliomo kwenye wimbo huu unakugusa au la.

No comments: