Friday, July 11, 2008

Kigogo fuska anaswa



Kufahamika huko kumekwenda sambamba na kunaswa kwa picha chafu zinazomuonyesha kigogo huyo ambaye ni mfanyabiashara maarufu jijini akiwa mtupu pamoja na Lola.

Awali vyanzo vyetu vya habari vilidai kuwa, Jonas alikuwa katika mgogoro wa kindoa kati yake na mkewe kufuatia uhusiano wake wa kimapenzi na mwanamuziki huyo, tuhuma ambazo alizikana.

Wakati gazeti hili likifuatilia skendo hiyo ya ngono, mfanyabiashara huyo alikuwa mbogo akikana kwamba hakupiga picha chafu na kwamba akiandikwa atachukua hatua.

Hata hivyo, siku chache baadaye mtandao wetu wa habari ulinasa picha za aibu zikimuonesha mwanaume huyo mwenye watoto kadhaa akiwa na kimwana wake chumbani na mkononi kashika simu.

Haijafahamika kama simu hiyo ndiyo iliyotumika kupiga picha hizo au la, lakini mazingira yanaonesha kwamba mfanyabiashara huyo alikuwa akifanya uchafu huo huku akijirekodi.

Aidha, habari kutoka kwa mmoja kati ya rafiki wa Lola zinasema kwamba, taarifa za picha chafu zilizochapishwa wiki jana zimemchanganya msanii huyo kiasi ca kutaka kunywa sumu.

No comments: