Saturday, March 29, 2008

MISS ABAKWA


Habari za kuaminika kutoka kwa rafiki wa karibu wa Miss huyo zilisema, kisa cha mrembo huyo kufanyiwa kitu mbaya kilitokana na utapeli alionao kwa wanaume, huku ulevi ukitajwa pia kumwingiza mtegoni.

Ilielezwa kuwa, usiku wa sikukuu ya Pasaka iliyoadhimishwa Machi 23, mwaka huu, ndani ya Ukumbi wa Travetine mrembo huyo alionekana akiwa na kijana mwenye asili ya kiasia akitumia naye kilevi.

“Tulikutana na (anataja jina la rafiki yake aliyebakwa) ukumbini, yeye alikuwa na kaka mmoja mhindi akanitambulisha kuwa ni rafiki yake,” alisema mtoa habari wetu ambaye jina lake linahifadhiwa na kuongeza kuwa hadi anaondoka aliwaacha wakiwa pamoja.

Aliongeza kuwa, siku ya pili usiku alipokea simu kutoka kwa rafiki yake (Miss) iliyomtaarifu kuwa hali yake ilikuwa mbaya na kwamba alihitaji msaada wa mawazo.

Ilielezwa kwamba, baada ya taarifa hiyo ndugu na jamaa walifika nyumbani kwa mrembo huyo na kumuuliza kilichomsumbua lakini kwa aibu alishindwa kuweka wazi kubakwa kwake hadi alipobaki na rafiki zake wa karibu ambao aliwaeleza ukweli.

“Alituambia kuwa alifanyiwa kitu mbaya na vijana wapatao wanne lakini aliyesuka njama hiyo alikuwa ni mtu wake aliyemtaja kwa jina la Hashim, huyo ndiye aliyemlewesha kisha kumpeleka gheto kwa rafiki zake,” kilisema chanzo chetu.

No comments: