Saturday, March 8, 2008

MAMISS WACHEZA MKANDA WA NGONO




Habari kutoka katika chanzo chetu cha kuaminika zinasema mastaa hao wa fani ya urembo walishawishiwa kucheza mkanda huo kwa malipo makubwa na kwamba usingeuzwa nchini.

“Yaani huwezi kuamini, nimeuona kwa macho yangu mwenyewe, ni uchafu mtupu! Warembo maarufu kama (anawataja majina) ambao hawana kashfa yoyote, wanaonekana katika mkanda huo wakifanya mambo ya ajabu,” kilieleza chanzo chetu.

Aidha chanzo hicho kiliendelea kupasha kuwa mkanda huo haupatikani nchini, lakini yeye alifanikiwa kuuona nyumbani kwa rafiki yake ambaye ni rafiki wa karibu sana na mmoja kati ya warembo walioshiriki kucheza muvi hiyo ya uchafu.

Hata hivyo baadhi ya warembo hao waliohojiwa na Ijumaa, waliruka madai hayo na kusema kuwa, wanaopakaza mambo hayo ni wabaya wao ambao hawapendi kuona mafan ikio waliyonayo katika urembo.

“Hizi habari umezitoa wapi? Lakini hazinishangazi sana, unajua watu hawapendi kuona mafanikio ya wengine ndiyo maana wanaamua kutuhusisha na mambo machafu ili kutiuharibia majina yetu,” alisema mmoja wa warembo waliohojiwa na gazeti hili.

Katika hatua nyingine, Miss Kanda ya Ziwa 2005, Maureen Gislasy ambaye pia anashikilia taji la mrembo anayevutia zaidi kwenye picha (Miss Photogenic) kwa mwaka huo, anadaiwa kutoswa na mpenzi wake wa kizungu raia wa Italia, baada ya kukataa kucheza mkanda mchafu.

Inadaiwa Maureen alipoambiwa na mchumba wake nia yake ya kumuoa, alianzisha mapenzi motomoto na mzungu huyo akijua fika kwamba kuolewa kupo njiani kumbe hakujua ana lake jambo.

Baada ya ndoa kukaribia kufungwa ndipo mtasha huyo alimuomba Maureen warekodi mkanda wa ngono ambao ungeuzwa Marekani na wao kulipwa fedha nyingi, ambazo zitawafanya waishi kwa raha mpaka mwisho wa maisha yao.

Inadaiwa Maureen aliamua kutokubali kurekodi mkanda wa ngono na ndoa isifungwe, kwa kile alichoona hata kama atalipwa fedha nyingi bado atakuwa amejidhalilisha.

Mafia ilipomsaka Maureen ili kujua kwa undani kile kilichopo, alikiri kutokea kwa tukio hilo na kuachwa na mchumba wake huyo kwa kitendo chake cha kukataa kurekodi mkanda wa ngono.

“Kweli dunia imeisha yaani kumbe hawa Wazungu wanawapenda mamiss kwa ajili ya kuwafanyia mchezo huu huku wakijifanya wanakumwagia fedha nyingi ili wakuchanganye akili.

“Mimi alinifuata na kuniambia anataka kunioa lakini baada ya muda akaanza kuniambia nirekodi mkanda wa ngono kwa ahadi za kunipa Sh milioni 50, lakini nilimjibu fedha inatafutwa na siwezi kupata utajiri kwa njia kama hizo huku nikimtisha akiendelea nitamshitaki,” alisema Maureen.

No comments: