Friday, November 11, 2011

KAFARA NZITO



Na Luqman Maloto
VIONGOZI wakuu wa Dini ya Shetani, Freemasons, wamefanya kafara nzito kuadhimisha kukamatwa, kuteswa kisha kuuawa kwa aliyekuwa Kiongozi wa Libya, Muammar Gaddafi.

Vyanzo vimesema kuwa ni kawaida kwa Freemasons kufanya sherehe yenye mrengo wa kafara kila mara, mpango wao unapofanikiwa sehemu yoyote ile.

Kwa mujibu wa mitandao kadhaa inayojihusisha na utoaji wa habari za jamii ya Freemasons, kafara ambayo hufanywa ni ile ya mnyama hususan mbuzi mwenye pembe zinazofanana na zile za jini anayeitwa Lucifer (jini mkuu) ambaye huabudiwa na wafuasi wa Dini ya Shetani.

Mnyama huyo huchinjwa kisha damu na kichwa chake huhifadhiwa kwenye chombo chochote chenye muundo wa ndoo ili pembe zitokeze kwa juu na kutengeneza alama maarufu ya Freemasons ambayo wafuasi wake huitumia kwa njia ya vidole kutoa salamu.

Habari zinasema Freemasons walifanya kafara hiyo usiku wa manane kwenye hekalu moja kubwa lililojengwa kwenye eneo la jangwa lililopo ndani ya Jiji la Misrata, Libya.

Inabainishwa kuwa viongozi mbalimbali wakubwa kwenye nchi zilizoendelea kiuchumi ambao wana vyeo vikubwa ndani ya jamii ya Freemasons, walihudhuria kafara hiyo.

MKAKATI HATARI
Habari zinabainisha kuwa Freemasons ipo kwenye mkakati thabiti wa kuitawala dunia kabla ya Desemba 2012.
Kutokana na mkakati huo, imebainishwa kuwa Freemasons wamekuwa wakiratibu sera zao kwa kuangusha utawala wa nchi mbalimbali ambao viongozi wake wameshindwa kuendana na matakwa yake.

Inaelezwa kuwa Gaddafi alikuwa kiongozi mwenye mrengo wa Kiislam japo alikuwa haweki wazi kwenye utawala wake na kwamba alikuwa anapingana vikali na Freemasons.

Kwa mujibu wa mnajimu msomi, Maalim Hassan Yahya Hussein, Jeshi la Kujihami la Umoja wa Nchi za Magharibi (Nato), hutekeleza mipango ya Freemasons kama lilivyofanya Libya kumng’oa Gaddafi.

Maalim Hassan ambaye ni mtoto wa aliyekuwa mnajimu maarufu barani Afrika, marehemu Sheikh Yahya Hussein, alisema kuwa dhumuni kuu la Freemasons ni kuzipiga vita dini za Kiislam na Kikristo.

“Ipo wazi kuwa wao lengo lao ni kuitawala dunia, kwa hiyo wanahakikisha hilo linawezekana kwa kudhoofisha Uislam na Ukristo ili ufe kisha Shetani ashinde hapa duniani,” alisema Maalim Hassan ambaye ni mrithi wa kazi za unajimu za marehemu Sheikh Yahya.

Aliongeza: “Mkakati mkubwa zaidi ni kuhakikisha dunia inaabudu Dini ya Shetani, wanataka kila mtu awe chini ya mamlaka ya jini mkuu (Lucifer). Dunia nzima itawaliwe na serikali moja na iwe na sarafu moja.”

Kauli ya Maalim Hassan inashabihiana na ile iliyopo kwenye maandiko kwamba zama za Dini ya Shetani kuishika dunia, kutakuwa na mfumo ambao utazuia mtu yeyote kupata huduma za kijamii mpaka awe mwanachama na atatambulika kwa chapa 666.

Habari zaidi zinaeleza kuwa Freemasons wanatumia njia mbalimbali kuhakikisha ulimwengu mzima hakuna anayeamini dini za Mungu na wanapambana kuhakikisha hata Yesu (Nabii Isa) atakaporejea akute hakuna aliye tayari kukombolewa.

Katika kuhakikisha wanapambana na nguvu ya Yesu, Freemasons wamekuwa wakitumia damu ndiyo maana hutoa kafara kwa kuchinja mnyama hasa mbuzi au kondoo wenye pembe kwa imani kwamba huwaongezea nguvu ya kuishika dunia.

Kutokana na tishio la Freemasons, viongozi wa kidini hususan wale wa Mashariki ya Kati, wamekuwa wakiwataka Waislam na Wakristo kwa imani zao, kufunga na kusali ili Dini ya Shetani isipate mafanikio inayoyataka.

SAKATA LA USHOGA
Habari zinasema kuwa Serikali ya Uingereza imekuwa ya kwanza kutumiwa na Freemasons katika kuhakikisha nchi zote zinazounda Jumuiya ya Madola zinapitisha sheria zinazokinzana na maandiko matakatifu yanayoaminiwa na waumini wa Dini za Kiislam na Kikristo.

Ushoga na usagaji ni vitendo ambavyo vinakemewa na dini hizo lakini hivi sasa, Freemasons wanadaiwa kuchochea mabadiliko ili watu wanaojihusisha na hulka hizo wawe huru kikatiba duniani.

Hivi karibuni, Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, alitangaza kuwa mwanachama wa Jumuiya ya Madola ili apate misaada inabidi kwanza aruhusu ndoa za jinsi moja (ushoga na usagaji) kwenye katiba ya nchi yake.

Tanzania ikiwa moja ya wanachama wa Jumuiya ya Madola, inapitiwa kwenye rungu hili, ingawa Balozi wa Uingereza nchini, Diana Corner alisema nchi yetu haihusiki.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alishatoa tamko kwamba Tanzania haipo tayari kuruhusu ndoa za mashoga na wasagaji kisha akaonya kuwa kauli ya Cameron inaweza kuivunja Jumuiya ya Madola.

SIYO FREEMASONS PEKE YAKE
Mbali na Freemasons, dini nyingine zenye mrengo wa Shetani ni Illuminati na Skull & Bones ambazo zinavuma zaidi Marekani.

VIGOGO WA FREEMASONS
Viongozi wanaotajwa kuwa vigogo wa jamii hiyo ni marais wa 43 na 44 wa Marekani, Barack Obama na George Bush, Rais wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy ambao wanaonesha alama za vidole ukurasa wa kwanza. Yupo pia Cameron na wengine wengi.

No comments: