Wednesday, January 13, 2010

Rais Kikwete alipotembelea Majeruhi Pemba!


Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma akimjulia hali mtoto Khamis Bakari(14) mkazi wa Wawi aliyelazwa kwenye hospitali ya Chake Pemba baada ya kujeruhiwa alipokuwa akijaribu kuingia katika uwanja wa michezo wa Gombani kuhudhuria maadhimisho ya sherehe za miaka 46 ya mapinduzi ya Zanzibar jana .Katika ajali hiyo mtu mmoja alipoteza maisha na wengine 18 kujeruhiwa na kulazwa katika hospitali hiyo ya chake ambapo Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Amani Abeid Karume na Waziri Kiongozi Shamsi Vuai Nahodha pamoja na viongozi wengine waliwatembelea majeruhi na kuwapa pole(picha na Freddy Maro)

No comments: