Thursday, June 18, 2009

Bajeti imejaa 'usanii'- Lipumba

Chairman wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba amesema Bajeti ya Serikali iliyowasilishwa bungeni wiki iliyopita na Waziri wa Fedha na Uchumi, Bw. Mustafa Mkulo imejaa usanii

Akiongea kwa kujiamini,Mh. huyo alisema bajeti hiyo imewasilishwa 'kisanii' kutoka chama cha 'kisanii' kinachoongozwa kwa 'usanii' mkubwa.

"Bajeti hiyo hakidhi mahitaji ya wananchi na inalenga kuwadidimiza na kuongeza umasikini nchini" alisema Prof Lipumba.

Alisema usanii kwenye bajeti hiyo ulianzia pale Serikali ilipotangaza kufidia hasara waliyopata wanunuzi wa mazao kwa msimu uliopita wa 2008/09 hasara hiyo ni kiasi cha sh. bilioni 21.9

Alisema Serikali italipia hasara hiyo ambayo imetokana na kushuka ghafla kwa bei ya mazao ya Tanzania katika soko la dunia wakati fedha hizo hazioneshwi katika vitabu vya bajeti.

Aliongeza kuwa hotuba ya Rais Kikwete aliyotoa mjini Dodoma hivi karibuni ya bajeti imeeleza kuwa serikali itatoa udhamini kwa mikopo inayofikia sh. bilioni 270 .


Alisema kuna hatari kuwa serikali inajiingiza kudhamini madeni ambayo hatimaye hayatolipwa na wanaodhaminiwa na kujiongezea mzigo wa madeni kwa nini madeni haya yadhamiminiwe kwa miaka miwili na sio mmoja?


"Wasi wasi wangu ni kwamba imeamua wadhaminiwe kwa miaka miwili ili watakaodhaminiwa wachangie kwenye kampeni za CCM,"alisema Prof. Lipumba.

No comments: