Thursday, April 2, 2009

Enzi zile alipoanza kutambulika rasmi ilitokana na wimbo wake uliokwenda kwa jina “Nipo Bize”.Si unakumbuka jinsi alivyokuwa akimwambia kimwana wake k


Enzi zile alipoanza kutambulika rasmi ilitokana na wimbo wake uliokwenda kwa jina “Nipo Bize”.Si unakumbuka jinsi alivyokuwa akimwambia kimwana wake kwamba asimtafute kwa sababu yuko bize?

Basi yawezekana ni kweli kwamba mshkaji huwa yuko bize kwani Jafarai ameshakamilisha albamu yake mpya itakayokwenda kwa jina Wali Nazi. Albamu hiyo itakuwa na nyimbo 9 ambazo zote zimerekodiwa katika studio za Fish Club za jijini Dar.Katika albamu hiyo Jafarai amewashirikisha wasanii wengine kama vile mwanadada Naazizi kutoka Kenya,Lamar ambaye pia ni producer wa albamu hiyo na pia Wateule.

Mojawapo ya nyimbo zilizomo katika albamu hiyo ni wimbo ambao unatamba katika vituo mbalimbali vya redio hivi sasa.Wimbo unaitwa Napenda Nini .Katika wimbo huu Jafarai ameshirikiana na mwanadada Fatma. Ni wimbo ambao una tungo kali,matata na ambayo nadhani ni huru kusema unaweza kuitafsiri unavyotaka wewe.Ni kazi nzuri ya sanaa ambayo inaonyesha jinsi gani lugha ya Kiswahili ni pana.

No comments: