Saturday, April 11, 2009

AMANI;ITADUMU?


Mojawapo ya mambo ambayo tunajivunia kama watanzania ni kuwa miongoni mwa nchi chache sana za kiafrika ambazo mpaka hivi leo viongozi wa upinzani na wale wa chama tawala hukutana pamoja,wakala,wakacheka na wakajumuika katika mambo mbalimbali ambayo yana mvuto au muelekeo wa kitaifa. Hapo sera huwekwa pembeni.Taifa kwanza.

Hili ni suala ambalo hatuna budi kujivunia…japo hilo basi.Wasiwasi nilionao ni kama amani hii,furaha hii,vicheko hivi vitadumu kwa muda gani.Nasema hivyo kwa sababu pamoja na vicheko,mwananchi wa kawaida bado anaumia.Bado anateseka.Hajaona faida wala matunda ya uhuru.Mpaka leo hii hata huo umeme unaogonga vichwa katika vyombo vya habari na mitaani yeye haujui.Hajawahi kutumia umeme! Kula yake ni ya kubahatisha.Pengo kati ya walionacho(mara nyingi kwa njia zisizo halali aka ufisadi) limekuwa kubwa kuliko Ngorongoro yetu.Hilo ni tatizo.Lapasa limkoseshe mtu usingizi.

Tunapocheka,tunapofurahi na tunapokumbushana kwamba tuna amani ni lazima tumkumbuke mwananchi…yule ambaye husahaulika magazetini,wilayani,mikoani na hata Bungeni. Tukifanya hivyo,tutakuwa na kila sababu ya kufurahi…kufurahi kwa pamoja! Vinginevyo…bora kununa

No comments: