Tuesday, January 20, 2009

KWANINI-NURU


Baada ya Walimwengu na Msela, mwanadada Nuru Magram (pichani) hapo jana amefyatua video ya wimbo Kwanini ambao ni miongoni mwa nyimbo 10 zinazotarajiwa kuwemo katika albamu yake aliyoipa jina Walimwengu. Albamu hiyo inatarajiwa kuingia sokoni mnano mwezi wa Machi mwaka huu.


Sikiliza mashairi yaliyomo katika wimbo huu,tazama jinsi hadithi iliyomo kwenye mashairi inavyosimuliwa katika video hiyo.Ukiiangalia kwa makini utagundua kwamba lipo jambo moja ambalo sio la kawaida linatokea katika mlolongo wa simulizi hilo.Sio la kawaida kwani katika simulizi hilo kuna mtu ambaye hafanyi kile ambacho wengi wetu tungetarajia afanye.Itazame kisha uniambie kama unaweza kuona nilichokiona mimi.Pata burudani.Kazi nzuri Nuru.

No comments: