Wednesday, November 16, 2011

Tanzania Yafungwa na Chad, Yapita Kwa Goli la Ugenini


Taifa Stars ambayo wiki iliyopita iliizamisha Chad 2-1 kwenye uwanja wake nchini Chad, imeshindwa kuwika nyumbani na kukubali kipigo cha bao 1-0.

Katika mechi iliyochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar esa Salaam, Taifa Stars ilifanikiwa kusonga mbele kwa faida ya goli la ugenini.

Chad walipata goli lao la ushindi kwenye kipindi cha pili dakika ya 48, mfungaji akiwa ni Mahamat Labbo ambaye ndiye aliyeipatia Chad goli lake la kufutia machozi kwenye mechi ya awali mjini N'Djaména.

Kwa matokeo haya, Taifa Stars imefanikiwa kuingia hatua ya makundi ambapo itashiriki katika kundi C lenye jumla ya timu nne zikiwemo Ivory Coast, Morocco na Gambia.

Fainali za Kombe la Dunia zinatarajiwa kufanyika mwaka 2014 nchini Brazil.

No comments: