Sunday, July 24, 2011

Warioba asema Bunge limekosa nidhamu

Mwandishi wetu

WAZIRI Mkuu Mstaafu, Joseph Warioba, amesema Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limekosa nidhamu na kwamba, linahitaji kuchukua uamuzi mgumu kurejesha hadhi yake.
Warioba alisema hivi sasa chombo hicho cha kutunga sheria kimegeuka kuwa sehemu vichekesho badala ya kujadili masuala muhimu ya kitaifa.
“Bunge limegeuka kuwa sehemu ya vichekesho, limekosa nidhamu linahitaji kuchukua uamuzi mgumu,” alisema Warioba.
Warioba ambaye alikuwa akizungumza na Televisheni ya Taifa (TBC1) jana asubuhi hakueleza kwa undani ukosefu wa nidhamu wa Bunge hilo.
Hata hivyo, matukio ya kila mara yanayoendelea kutokea bungeni ikiwamo kuzomeana, kuzungumza ovyo bila mpango na kuwapo kwa madai ya rushwa ni moja ya mambo yalimfanya atoe kauli hiyo.
Vurugu zinazotokea bungeni mara kadhaa zimekuwa zikimfanya Spika na wenyeviti wa vikao vya Bunge kuwa katika wakati mgumu kusimamia mijadala.
Mara kadhaa Spika amekuwa akisikika akikemea tabia hiyo hadi wakati fulani alifikia kuwalingananisha na watu wa sokoni Kariakoo.
Hata hivyo Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema alisema wabunge kusingana bungeni si jambo la jabu sana na kwamba ni dalili ya kuelekea kwenye demokrasia kamili bungeni.
Warioba ni Waziri Mkuu Mstaafu wa kwanza kulinyoshea kidole moja kwa moja Bunge katika siku za hivi karibuni.
Moja ya kashfa ambazo hivi karibuni zimelighubika Bunge ni pamoja na baadhi ya wabunge kutuhumiwa kuchukua rushwa ili waweze kupitisha bajeti na miongoni mwa zilizotajwa ni ya Wizara ya Nishati na Madini.
Kashfa hiyo ndiyo iliyosababisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, David Jairo, kuingia katika kitanzi cha kuhusishwa kwake na kuandika barua kwenye taasisi zilizo chini ya wizara yake kuomba fedha za kupitisha bajeti hiyo.
Kashfa nyingine ya Bunge ni lile tukio la wabunge kuzomeana na kumfanya kila mbunge kuwasha kipaza sauti kuongea bila ya kufuata taratibu.
Lawama nyingine dhidi ya Bunge ni ile iliyoibuliwa na Mbunge wa Nyamagana, Ezekiel Wenje ya kutuhumu Kamati ya Bunge kuwa ilifanya mambo kinyume cha taratibu.
Zipo hoja nyingine ambazo ziliibuliwa na kusemwa bungeni zikionya kuwa, Bunge limekuwa likitumika kama ‘rubber Stump’ (mhuri) ya kupitisha mambo mbalimbali bila kuyafanyia uchunguzi wa kina na kujiridhisha.
Warioba akizungumzia Katiba Mpya alisema muswada uliopo katika mchakato umesahau mambo muhimu, kama vile ya uchumi na maendeleo ya jamii badala yake una mambo mengi ya kisiasa.
Alisema masuala mengi yaliyomo ndani ya muswada huo yanalenga kulinda maslahi ya wanasiasa na kuacha kuzungumzia masuala muhimu kwa maendeleo ya wananchi.
Warioba ambaye pia ni Jaji Mstaafu, mara kwa mara amekuwa akitoa kauli nzito za kuishauri Serikali katika masuala ya rushwa na utawala bora.
Mwaka jana, Jaji Warioba alionya dhidi ya mwelekeo wa uongozi nchini kununuliwa kama bidhaa kutokana na vitendo vya rushwa vilivyokuwa vikifanyika karibu na Uchaguzi Mkuu.
Alisema: “Kwa jumla sasa uongozi wa nchi unaanza kubinafsishwa kama biashara ambayo wenye fedha ndiyo watafaulu. Kwa kifupi fedha
SOURCE:Mwananchi

No comments: